PROFESA NDALICHAKO AZINDUA MRADI WA 200BLS JIJINI ARUSHA. - Mazengo360

Breaking

Wednesday, 23 August 2017

PROFESA NDALICHAKO AZINDUA MRADI WA 200BLS JIJINI ARUSHA.

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako  leo amezindua mradi wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 200 unaojulikana kama Elimu na Ujuzi kwa ajili ya kazi na uzalishaji, (ESPJ) kwenye Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyopo mkoani Arusha.

Waziri wa Elimu ,Mafunzo na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akizindua mradi wa Vituo vya Umahiri utafiti wa kilimo na Magonjwa ya binadamu pamoja na mradi wa kuongeza ujuzi kwa kazi za uzalishaji zinazoleta tija,kulia ni Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa Ukanda wa  nchi  za Tanzania, Malawi , Burundi na Somalia Bi Bella Birds na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo.

Akizungumza katika uzinduzi huo Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa miradi hiyo itasaidia kuongeza rasilimaliwatu yenye ujuzi wa kati ambao watafanya kazi katika sekta za kilimo,Utalii,Ujenzi ,nishati na madini watapatikana kwa wingi.

Alisema kuwa Miradi iliyofadhiliwa ni pamoja na vituo vine vya umahiri katika masuala ya utafiti wa kilimo na magonjwa ya binadamu,ikiwemo viwili vinavyomilikiwa na Chuo Kikuu cha Technolojia cha Nelson Mandela cha Arusha pamoja na vituo vingine viwili vilivyopo katika Chuo cha Kilimo cha Sokoine University of Agriculture cha Morogoro.


Waziri wa Elimu ,Mafunzo na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akiandamana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo (kushoto) na viongozi wengine, akiwasili katika Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela cha Arusha ambapo amezindua mradi wa Vituo vya Umahiri utafiti wa kilimo na Magonjwa ya binadamu pamoja na mradi wa kuongeza ujuzi kwa kazi za uzalishaji zinazoleta tija uliofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa ukanda wa nchi za Tanzania, Malawi, Burundi na Somalia Bella Birds amesema, uboreshwaji wa rasilimali watu kwa kuongeza ujuzi uliokosekana utasaidia taifa kufikia malengo yaliyokusudiwa na baadae kufikia uchumi wa viwanda.

Mkurugenzi huyo amesema pia kwamba, inakadiriwa kuwa Vijana takribani zaidi ya milioni 1 huitimu katika vyuo na kuingia katika soko la Ajira kila mwaka hivyo anatarajia kuwa nafasi za ajira kwa vijana hao zitatengenezwa na sekta binafsi iwapo zitashirikiana vyema na serikali .

Nae Makamu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela, Karoli Njau alisema kuwa mradi huo utasimamiwa kwa makini ili kuhakikisha kuwa malengo yanafikiwa hususan katika vituo vya umahiri pamoja na mradi wa ujuzi.


Waziri wa Elimu ,Mafunzo na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akimshukuru Mkurugenzi wa Benki ya Dunia katika Ukanda wa Tanzania, Malawi, Burundi na Somalia Bi Bella Birds mjini Arusha katika Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandelea mara baada ya kuzindua mradi wa thamani ya shilingi bilioni 200  utakaowanufaisha watanzania wengi hapo jana.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi  Tanzania (TPSF) Godfrey  Simbeye ameeleza pia kwamba TPSF ina upungufu mkubwa wa watu wenye ujuzi nchini ambapo huchangia kutokukidhi mahitaji ya soko la ajira.
Bwana Simbeye aliongeza zaidi kwa kubainisha kwamba, waajiri hulazimika kuajiri watu wenye ujuzi kutoka nje ya nchi jambo linalogharimu fedha nyingi, hivyo mradi huo utasaidia vijana zaidi ya 30,000 kupata ujuzi utakaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

MWISHO.


No comments:

Post a Comment