SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar
imezindua mpango kazi wa miaka mitano wa kudhibiti vitendo vya ukatili na
udhalilishaji kwa wanawake na watoto ambapo umelenga kurejesha hadhi na heshima
ya mwanamke na mtoto katika jamii.
![]() |
Waziri
wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar, Mhe Mandline Cyrus Castico akisoma kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Dkt
Ali Mohamed Shein, taarifa ya uzinduzi wa
mpango wa serikali wa miaka mitano wa kudhibiti vitendo vya unyanyasaji kwa
wanawake na watoto mjini Zanzibar hivi leo.
Akizindua
mpango huo leo mjini Zanzibar kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Mhe Dkt Ali Mohamed
Shein, Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe Maudline Cyrus Castico amesema, Serikali
imezindua mpango huo kwa kuwa inathamini utu wa raia wa Zanzibar.
Waziri Maudline
alieleza pia kwamba, mpango huo umeweka mikakati imara na madhubuti ya
kudhibiti vitendo vyote vya kikatili na vya udhalilishaji kwa wanawake na
watoto mfano kupigwa, kudhalilishwa kingono, kubakwa kwa wanawake na watoto na
mengine yanayofanana na hayo, alieleza zaidi Mhe Waziri Mandline.
Pia, serikali
imetoa rai kwa vyombo vyote husika katika mpango huu likiwemo jeshila polisi
kushirikiana kwa pamoja ili kutekeleza mpango huo ili azma iliyokusudiwa na
serikali itimie.
Akisoma risala
yenye ujumbe toka kwa watoto wa Zanzibar mtoto Jaffar Ahmad alisema
kupitia risala hiyo, vitendo vya ukatili na udhalilishaji wanavyofanyiwa
na jamiii inayowazunguka vimekuwa vikiwaumiza kisaikolojia na kuwarudisha nyuma
katika masomo na hata kusababisha wasifurahie haki yao kama watoto katika jamii.
Risala hiyo pia
ilibainisha wazi aina ya vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watoto, vikiwemo
kupigwa, kulawitiwa, kuchomwa moto baadhi ya sehemu za viungo vya mwili pamoja
na vichanga kutupwa ovyo kama mizoga, risala yao ilifafanua hayo.
Aidha watoto
imeiomba serikali kushirikiana na
mashirika ya kimataifa pamoja na wadau wengine wa haki za binadamu pamoja na wale
wa maendeleo hapa nchini, ili
kusimamia na kuwachukulia hatua madhubuti wale wote watakaobainika
kuendeleza vitendo vya udhalilishaji na kisha kuwafikisha katika vyombo vya
sheria.
Nae Fatma
Abdalla Mussa akisoma risala ya wanawake wa Zanzibar ameitaka serikali
kuyafanyia kazi na kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya udhalilishaji
yanayowakumba wanawake wa jamii ya Zanzibar.
Ujumbe huo wa
wanawake pia umebainisha baadhi ya vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa vikiwemo
kutelekezwa wao na watoto majumbani na waume zao.
Wameeleza
vitendo vingine ni pamoja na kupigwa, kubakwa na hata kunyimwa haki ya kumiliki
au kurithi mali walizochuma na wenzi wao pindi wanapotengana katika ndoa au
mmoja wao kufariki.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment