WATU
mbalimbali nchini Uingereza wanaojihusisha na mchezo wa soka wamempongeza nguli
wa mchezo huo Wayne Rooney kwa kulitendea haki soka la Uingereza na kusema
anastahili tuzo ya heshima.
![]() |
Wayne Rooney akishangilia moja ya magoli aliyoifungia timu ya Taifa ya Uingereza, |
Kwa mujibu wa gazeti la Uingereza la “The Telegraph,” mwenyekiti wa FA, Greg Clark amemtaja Rooney kama alama ya Taifa la Uingereza katika soka na kuongeza kuwa alilitendea haki soka la Taifa hilo.
Wayne Roone, 31, ambae
ametangaza kustaafu soka katika timu ya Taifa ya Uingereza ingali bado akiwa
katika kiwango cha ujana wake baada ya kurejea katika timu yake ya Everton
ambapo hadi anatanga kustaafu ameshaifungia club hiyo magoli mawili kwenye msimu
huu wa ligi ya premier.
![]() |
Wayne Rooney akishangilia baada ya kuifungia goli timu yake ya Everton katika ligi ya Premier. |
Nae mwandishi nguli wa
habari za michezo nchini Uingereza Alan Tyers amemwagia sifa Rooney kwa umairi
aliouonyesha wakati wa mchezo kwa kizazi chake, ambapo pamoja na nguli wengine
Rooney aliweza kuiletea sifa Uingereza katika medani ya soka na sasa ameacha
heshima kubwa.
Wengine aliocheza nae
katika timu ya Taifa ya Uingereza ambao wote wameshastaafu soka ni pamoja na
Owen, David Beckham, Stephen Gerald na Frank Lampard. Wengine ni Paul Scholes
na Rio Fernandes.
Rooney alianza kuchezea
timu ya Taifa ya Uingereza mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 18, nakufanikiwa kuisaidia
Uingereza kuingia kwenye robo fainali ya Europian Championship.
Amestaafu soka kwenye timu
ya Taifa ya Uingere akiwa na rekodi ya mabao 53 huku akishuka dimbani mara 119
akiwa na timu yake ya Taifa ya Uingereza.
(Taarifa na picha, kwa
mujibu wa The Telegraph la Uingereza).
MWISHO.
No comments:
Post a Comment