TANZANIA KUENDELEA KUWA KITOVU CHA KISWAHILI DUNIA. - Mazengo360

Wednesday, 6 September 2017

TANZANIA KUENDELEA KUWA KITOVU CHA KISWAHILI DUNIA.

SEREKALI ya Tanzania imesema itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kukuza lugha ya Kiswahili katika ukanda wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki na kutoa walimu wa lugha hiyo katika mataifa mengine duniani.

SAMIA+PX+1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe Samia Suluhu Hassan akihutubia kongamno la kwanza la Kiswahili la nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki lililoanza leo mjini Zanzibar.

Akihutubia wajumbe wa Kongamano la kwanza la Kiswahili la nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suhulu Hassan amesemaKiswahili ndio nyenzomuhimu ya kuwaunganisha wote.

Mhe Samia aliendelea kusema zaidi kwamba, Tanzania itabakia kuwa msaraei wa mbele katika kukuza na kudumisha Kiswahili katika Ukanda huu na kuongeza kwamba ipo tayari kutoa walimu wa Kiswahili katika nchi majirani.

Amezitaja nchi hizo ikiwemo Sudan ya Kusini na mataifa mengine yanayohitaji walimu ili kufanya lugha ya Kiswahili inazidi kuenea zaidi na kuzungumzwa katika ukanda huu mzima na hata ulimwenguni kote.

Pia Mhe Samia ameeleza kwamba, kufanyika kwa kongamano hilo lakwanza la Kiswahili katika ukanda huu mjini Zanzibar ni kuthamini mchango mkubwa wa lugha hiyo ambapo inafungamanishwa na umuhimu wa  kihistoria ambapo nimwanzo mzuri wa Kamisheni ya Kiswahili katika kutekeleza kazi zake, alifafanua Makamu wa Rais.

SAMIA+PX+2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua kongamanola kwanza la Kiswahili la Afrika Mashariki hivi leo mjini Zanzibar. Wengine kushoto kwake ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (Tanzania Bara) Mhe Dkt Harson Makyembe, na kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiwahili ya Afrika Mashariki Prof Kenneth Simala (suti ya ugoro) akifuatiwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Dkt Augustine Maige.

Aidha, Mhe Samia ameeleza kwamba serikali za nchi wanachama wa jumuya ya Afrika mashariki zijitahidi kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kuiwezesha kamisheni hii ya Kiswahili ili iweze kutekeleza mapendekezo ya kisera yatakayotolewa baada ya kongamano hilo.

 Kongamano la kwanza la kamisheni ya kishwahili jumuiya ya Afrika Mashariki litaendelea kwa mfululizo kwa siku mbili mjini Zanzibar ambapo limeshirikisha jumla ya wajumbe zaidi 150 kutoka nchi za ukanda huu pamoja na wawakilishi wa baadhi ya nchi nyingine barani Africa wakiwemo waadhiri wa vyuo vikuu na waandishi mbalimbali wa habari.

MWISHO.