VIGOGO SERIKALINI WAVULIWA NGUO RIPOTI YA ALMASI. - Mazengo360

Wednesday, 6 September 2017

VIGOGO SERIKALINI WAVULIWA NGUO RIPOTI YA ALMASI.

KAMATI teule ya bunge iliyoundwa na Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai leo imewasilisha ripoti zake mbili huku ikiwataja vigogo serikali kuhusika katika ufujaji mkubwa wa madini ya Almasi.

ALMASI+CHAWENE
Mhe George Simbachawene, Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI nae ameguswa na ripoti ya Bunge kuhusu madini ya Almasi iliyowasilishwa Bungeni leo mjini Dodoma.

Ripoti hizo mbili zilizowasilishwa leo bungeni mjini Dodoma ziwataja baadhi ya mawaziri wa Nishati na Madini wa sasa na wa zamani kuhusika kwa kiasi kikubwa katika kinachoaminika kuwa ni uzembe wa makusudi uliousababishia tena serikali hasara kubwa.
Waliotajwa katika ripoti hizo ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa zamani wa Nishati na Madini Mhe William Ngeleja na mwenzie aliyemfuatia ofisini aliyekumbwa na kashfa ya ESCROW na ile ya makinikia ya ACACIA Mhe Prof Sospeter Muhongo.
Wengine wapya walioongezeka katika orodha ya sasa ni pamoja na Mhe George Simbachawene, ambaye kwa sasa ni Waziri wa TAMISEMI, ambaye pia alishawahi kuwa Waziri katika Wizara hiyo ya Nishati na Madini pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TMAA  na Mwenyekiti WA Kamati Teule ya Rais ya kuchunguza Makinikia ya ACACIA Prof Abdilkarim Mruma.

ALMASI+CHAWENE+3
Mwenyekiti wa Kamati  hiyo Mhe Musa Azzan Zungu.

Pia wengine wamo Mhe Edward Ngonyani pamoja na Mwanasheria aliyejiuzulu pia katika kashfa ya ESCROW Mhe Fredrick Werema.
Katika kamati ya uchunguzi wa Almasi iliyowasilishwa na Mwenyekiti wake Mhe Mussa Azzani Zungu (Mbunge wa Ilala-CCM) kamati hiyo imeeleza kusikitishwa na kampuni ya uchimbaji wa almasi kumzawadia kiongozi mmoja mkubwa ambaye alikuwa serikalini (Haikutaja jina) almasi yenye thamani ya dola milioni 20.
Ripoti hiyo pia imesema taratibu za uchimbaji wa almasi hapa nchini unafanywa kiholela huku kampuni nyingi zikiwa  vinara wa kukwepa kulipa kodi serikalini kwa  kubadilishana majina ya makapuni kwa madai ya kusingizia kupata hasara ili kukwepa kodi, ripoti ilieleza.
Akizungumzia kampuni ya uchimbaji wa madini ya Williamson Diamond, ripoti imesema tangu mwaka 2007 hadi 2017 haijawai kulipa mapato yeyote serikalini kwa kulipa kodi.
Amesema kuwa kuwa kampuni hiyo haikuweza kulipa kodi na Mrabaha kwa kisingizio kuwa kampuni inapata hasara,huku ripoti hiyo  ikihoji kwamba kama kweli kampuni inapata hasara kwanini isitangaze kufilisika nakuondoka.
Alisema licha ya kuwa almasi ya Tanzania kuwa bora kuliko sehemu nyingine lakini bado serikali imekuwa hainufaiki na jambo lolote kutokana na madini ya almasi.
ALMASI+CHAWENE+2
Waziri wa Zamani Mhe Prof Sospeter Muhongo.

Kamati ya Zungu imempata Prof.Mruma na hatia ya kuruhusu madini ya Almasi yapotee kizembe wakati akiwa Mwenyekiti wa bodi ya uwakala wa ukaguzi wa madini Tanzania (TMAA).
Zungu alisema Profesa Mruma alipohojiwa aliiambia kamati kwamba alisaini bila kusoma kwa undani nyaraka husika.
Alipoulizwa kwanini alisaini bila kusoma, alisema alikuwa 'busy' sana na hivyo hakupata muda wa kusoma nyaraka hizokwa kina na hivyo aliamua kusaini kwa kuwa amini watendaji wa wizara waliokuwa chini yake.
Kamati zote mbili zimempata Mhe George Simbachawene na hatia ya kusaini Mikataba yenye madudu mengi yaliyoingiza nchi yenye kuleta  hasara kubwa.
Simbachawene ni moja wa watu ambao walisha wahi kufanya kazi Shirika la STAMICO.
Aidha Zungu amesema kuwa Prof Muhongo nae alisaini mkataba wa Tanzanite na kampuni ya TML licha ya kushauriwa na mwanasheria mkuu na mwanasheria wa wizara asisaini.
MWISHO.