WENGI WAKESHA WAKIMUOMBEA TUNDU LISSU. - Mazengo360

Thursday, 7 September 2017

WENGI WAKESHA WAKIMUOMBEA TUNDU LISSU.

KATIKA hali inayoonyesha mapenzi makubwa kwa Mhe Tundu Lissu Rais wa TLS na Mbunge wa Singida Mashariki-CHADEMA, utafiti unaonyesha wengi wamekesha kumwombea afya njema usiku wa leo.

Tumwombee+lISU
Mhe Tundu Lissu, Rais wa TLS na Mbunge wa CHADEMA.

Mhe Tundu Lissu aliyeshambuliwa na watu wasiojukana kwa risasi alipokuwa akiingia nyumbani kwake mjini Dodoma eneo la Area D jana mchana akitokea bungeni, taarifa ya mapema usiku huu imeeleza afya yake inaendelea kuimarika na amehamishiwa jijini Nairobi Kenya kwa matibabu zaidi.

Taarifa aliyoitoa usiku huu wa manane akiwa uwanja wa ndege wa mjini Dodoma wakati wa kuondoka kwenda Nairobi Kenya, Mbunge wa Iringa Mjini-CHADEMA Mhe Peter Msigwa amesema afya ya Mhe Tundu Lissu inaendelea kuimarika baada ya kutoka chumbacha upasuaji.


tunduu+ndege
Mhe Tundu Lissu akiingizwa kwenye ndege ya kukodi  katika Uwanja wa Ndege wa  mjini Dodoma usiku huu  ambapo alipelekwa jijini  Nairobo Kenya kwa matibabu zaidi.

Amesema, “Napenda kuwajulisha kwa mara nyingine tena kwamba Lissu wetu anaendelea vizuri. Ametoka chumba cha upasuaji na hali yake inaendelea kuimarika” ilieleza taarifa hiyo fupi ya twitter ya Mhe Msigwa mapema usiku huu.
Mhe Msigwa pia amewataka watu wote wenye mapenzi mema na Mhe Tundu Lissu wamchangie fedha zitazosaidia kugharimia matibabu yake nje ya nchi kupitia mtando wa simu ya VODACOM kupitia M-PESA No. 0759-865 786 ya Ester Matiko, Mbunge-CHADEMA Jimbo la Tarime mjini.

Nae Kikwete Ridhiwani ambaye ni Mbunge wa Chalinze-CCM amefanya maombi maalum ya kumwombea afya njema Mhe Tundu Lissu na kumsii Mungu amponye haraka arudi katika majukumu yake.

Ndege+Tundu+Lissu
Ndege ya kukodi iliyo msafirisha Mhe Tundu Lissu kwenda jijini Nairobi Kenya usiku wa kuamkia leo ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma muda mfupi kabla ya kuondoka.

Kikwete alisema katika sala yake akisema,  
Ridhiwani+2
Mhe Ridhiwani Kikwete (Mb)

“Mungu Baba uliyeahidi kuipenda Tanzania na watoto wake, timiza upendo wako. Mjalie kaka yetu Lissu afya na uzima, amina!!” Kikwete alimalizia maombi yake.

Inavyoonyesha Mhe Tundu Lissu anapendwa na wengi ndani na nje ya Tanzania na watu wote bila kujali umri, elimu, kipato, jinsia wala cheo ambapo mtandao huu usiku kucha umekua ukifuatilia kwa karibu salamu zote za matashi mema kwake kupitia mitandao ya facebook, twiiter na mingineyo, ambapo matokea yanaonyesha wazi kwamba Mhe Tundu Lissu anapendwa zaidi na watu wote.

Salamu alizozituma Rais wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kupitia mtandao wake wa twitter, amelitaka jeshi la polisi kuwasaka na kuwatia nguvuni wale wote waliohusika kumjeruhi kwa risasi Mhe Tundu Lissu na kuwafikisha haraka katika mikono ya sheria.

Rais Dkt Magufuli amesema zaidi katika twitter yake fupi kwamba, anamwombea afya njema Mhe Tundu Lissu ili arejee haraka katika afya na kazi zake, alimalizia Mhe Rais Dkt Magufuli.

Navyo vyama vya kisheria na haki za binadamu katika ukanda wa nchi za Maziwa Makuu za Afrika Mashariki nazo zimetuma salamu zao za kimaandishi kwa CHADEMA na kwa Mhe Tundu Lissu na kulaani vikali tukio la kushambuliwa kwake.

Chama cha wanasheria cha Kenya yaani “The Kenya Law Society-KLS nacho kimetuma taarifa yake ya maandishi iliyo sainiwa na Rais wa KLS Mwanasheria Isaac N. Okero, imelaani vikali shambulizi hilo.

Mhe Okero ameeleza katika taarifa yake kwa Rais wa TSL kwamba “Shambulio hilo ni la kidhalimu na ni dhidi ya Utawala wa Sheria na hivyo linapaswa kupingwa na kulaaniwa kwa nguvu zote, hivyo kumwombea Mhe Tundu Lissu apone haraka” ilimalizia taarifa hiyo ya KLS.

Nae Naibu Mkurugenzi wa chama cha kutetea haki za binadamu (Amnest International) Ukanda wa nchi za Maziwa Makuu, Madam Sarah Jackson nae kimewasilsha salamu maalum za maandishi kumtakia kheri apone haraka Mhe Tundu Lissu.

Taarifa hiyo ilitoa wito kwa mamlaka husika yaani Serekali ya Tanzania, kufanya kila njia kuwatia nguvuni wale wote waliohusika kumshambulia Mhe Tundu Lissu ili isionekane kwamba shambulio hilo si la kisiasa, taarifa hiyo imemalizia.

Navyo vyama vya siasa hapa nchini havikubaki nyuma kumwombea na kumtakia afya njema Mhe Tundu Lissu,baada ya shambuliohilo zilizotolewa usiku wa kuamkia hivi leo.

Taarifa ya maandishi iliyotumwa kwa CHADEMA kumtakia Mhe Tundu Lissu nafuu ya mapema na kulaani vikali shambulio hilo, salamu za Chama cha Mapinduzi-CCM ilizosainiwa na Katibu Mwenezi wake Mhe Humfrey Polepole zimelaani vikali kitendo hicho.

Taarifa hiyo ya CCM imeendelea kusema kwamba, “imepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kushambuliwa kwa risasi Mhe Tundu Lissu,Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa TLS, Polepole alifafanua.

Nacho chama cha ACT-Wazalendo kinachoongozwa na Mhe Zitto Kabwe kimetuma taarifa yake ya maandishi kwa CHADEMA iliyosainiwa na Katibu Mwenezi wa chama hicho Bwana Ado Shaibu.

Tarifa ya ACT-Wazalendo imewataka watanzania wote kuungana pamoja kumwombea kwa Mungu Mhe Tundu Lissu ili apone haraka ili arejee katika majukumu yake, taarifa ya ACT-Wazalendo ilimalizi.

Katika jambol linaloonyesha Mhe Tundu Lissu anapendwa na wengi, taarifa takribani katika mitandao yote ya kijamii usiku huu zilikuwa zikizungumzia taarifa ya kushambuliwa kwa risasi Mhe Tundu Lissu.


Ndugai
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akiongea na Vyombo vya Habari jinsi alivyopokea taarifa ya kushambuliwa Mhe Tundu Lissu alipokuwa njiani akirejea mjini Dodoma akitokea jijini Dar alipohudhuria kukabidhiwa ripoti ya Uchunguzi wa Madini kwa Mhe Rais Dkt Magufuli na Waziri Mku Mhe Kassim majaliwa Ikulu hapo jana.

Wengi wa wachangiaji katika mitandao bila kujali makundi yao wala itikadi zao wamekuwa wakilaani kwa kiasi kikubwa kitendo hicho na kumwombea ili apone haraka.

“Tuseme kwa ufupi taarifa ya Mhe Tundu Lissu imefunika kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari”, imethibitika hivyo.

Mhe Tundu Lissu amesafirishwa kupelekwa Nairobi Kenya kwa matibabu zaidi usiku wa kuamkia leo kwa ndege maalum ya kukodi, ambapo Mhe Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa Upinzani Bungeni pamoja na mkewe Tundu Lissu pamaoja na viongozi wengine wa kambi ya upinzani bungeni waliandamana katika msafara huo.

Wakati huo huo viongozi wengi Serekalini, Bungeni na pamoja na watu mbalimbali wameonekana kuguswa sana na tukio hili nakushiriki kikamilifu kumjulia hali Mhe Tundu Lissu mara alipofikishwa hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma hapo jana.

Gari+ya+Lissu
Gari ya Mhe Tundu Lissi iliyoshambuliwa kwa risasi zaidi ya tano,na kumjerui vibaya.

Japo viongozi wengi wa Serekali kuwepo jijini Dar es Salaam kuhudhuria kukabidhiwa kwa ripoti ya Bunge ya Uchunguzi wa Madini ya Tananate na Almasi, wengi wao walirejea mjini Dodoma haraka ili kuwa kumjualia hali Mhe Tundu Lissu wakiongozwa na Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto  Mhe Ummy Mwalimu pamoja na Katibu Mkuu wake Dkt Ulisubisya na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na madaktari wengine wote, walishirikiana vizuri na kufanya kazi ya kumpatia matibabu ya awali Mhe Tudu Lissu ili damu isivuje kwa wingi katika majeraha ya risasi na kuweza kuokoa afya ya Mhe Tundu Lissu pindi alipofikisha hospitalini hapo.


MWISHO.