RAIS
Dkt
John Magufuli amesema “Sikuja Serekalini kutafuta mchumba, bali kuwatumikia
watanzania na hivyo sipo tayari kuona mali za watanzania zikiporwa kwa kumwonea
mtu aibu kwa kumlinda”
Rais Dkt Magufuli leo
amekuja kivingine kabisa wakati wa kupokea ripoti mbili maalum za kamati ya
bunge juu ya uchunguzi wa madini ya Tanzanate na Almasi iliyowasilishwa kwake na
Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa Ikulu jijini Dar.
Rais kupitia hotuba yake aliyoitoa
na kurushwa moja kwa moja na vyombe mbalimbali vya habari kwenda kwa watanzania
wote, leo ameonyesha kuwa mpole na mwenye subira zaidi katika hotuba yake
lakini yenye ujumbe mzuri,mpana kwa watanzania.
Rais aliyasema hayo leo
baada ya kukabidhiwa ripoti hizombili na Mhe Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ikulu
jijini Dar nakuonyesha kusikitishwa mno na baadhi ya wateule wake kutajwa
katika kashfa hii ambapo yeye ameeleza
wazi kwamba ni kukosa uzalendo kwa taifa letu kwa kiwango kikubwa.
Ripoti hizo mbili ni matokeo
ya kazi nzuri iliyofanywa na bunge baada ya Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai
kuunda kamati maalum ili kuchunguza mwenendo wa uchimbaji madini ya Tanzanate
na Almasi hapa nchini.
Tunaungana watanzania wote
wenye nia njema kwa Taifa letu la Tanzania kumpongeza Mhe Rais Dkt John Pombe
Magufuli kwa namna alivyokuja mbele ya umma hivileo na kuwaelezea jinsi Taifa
linavyofilisiwa na baadhi ya watanzania waliokabidhiwa na wengine amewateua
yeye kusimamia rasilimali zetu watanzania.
Rais leo katika hotuba yake
ameonekana mpole, mtulivu lakini mwenye kubeba hisia kubwa ya kutaka kuchukua
hatua za kurekebisha mwenendo wa watendaji serekalini.
Rais amekuja tofauti kabisa
na wakati ule alipopokea ripoti ya makontena ya mchanga wa makinikia wa ACACIA.
Rais amesikitishwa zaidi
hususani aliposikia hata baadhi ya waliotajwa katika ripoti hizi mbili wapo wateule
wake aliowaamini sana ambapo ndio sababu haswa ya yeye kuonyesha subira ile
kubwa hivi leo.
Baadhi ya waliotajwa katika
ripoti hizo ni pamoja na Waziri katika ofisi yake anaye shughulikia na
usimamizi wa Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe George
Simbachawene, ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe-CCM, toka Mkoani wa
Dodoma.
Mteule mwingine ambaye
ametajwa katika ripoti hizi kwa sasa ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Mhe Edwin Ngonyani.
Viongozi hawa wawili
waandamizi ambao ni wateule wa Rais ni wazi wamemuaibisha mno Mhe Rais na hadi
kumfanya awe mpole na mwenye umakini wa kuzungumza katika hotuba yake.
Rais amewaomba radhi sana
watanzania kwa vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wanaokabidhiwa
wajibu wa kusimamia rasilimali za watanzania na kuwataka wale wote waliotajwa
katika ripoti hizo kuachia nafasi zao ili kupisha uchunguzi ambao Idara ya
TAKUKURU imekabidhiwa kuianza rasmi.
Jambo la pili ambalo Rais
Dkt Magufuli ameonyesha utofauti kabisa wakati huu ni hatua yake ya kuwapongeza
waziwazi wabunge wa upinzania walioshirikishwa katika kamati hiyo ya bunge.
Rais amesikakia akisema
wazi kwamba, “watanzania tuache tofauti zetu za kivyama au kiitikadi tuangalie
uzalendo kwa nchi yetu”, huku akimtaja kwa jina mbunge wa upinzani wa Jimbo la
Momba kupitia CHADEMA Mhe Silinde.
Katika hili Rais Dkt
Magufuli amedhihirisha wazi kwamba yeye ni baba wa wote, bila kuchagua
mwana-CCM au mpinzani ila ni Rais wa watu wote.
Hakika hapa Rais ameonyesha
uzalendo wa hali ya juu hususani kwa kukubali kwamba sote ni watanzania na kila
mtu anaweza kulitumikia taifa lake kikamilifu bila kujaliitikadi zake kivyama
endapo watapatiwa nafasi ya kufanya hivyo.
Hapo jana wakati wa kamati
ikikabidhi ripoti zake mbili kwa Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai na baadae pia
kuzikabidhi kwa Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, kiongozi wa kambi ya upinzani
bungeni na mbunge wa Hai Mhe Freeman Mbowe (CHADEMA) alimpongeza Spika kwa
hekima kubwa ya kiuongozi aliyotumia na kuwashirikisha wabunge wa vyama vyote
bila kubagua, jambo ambalo ni zuri na wakatekeleza jukumu hilo vizuri,
alielezea Mhe Mbowe katika hotuba yake.
Aidha, ni imani ya
watanzania wote kwamba muhimili wa mahakama nao utatekeleza wajibu wake hapo
baadae wakati TAKUKURU itakapokamilisha wajibu wake wa uchunguzi kama mihimili
hii miwili ya serekali na bunge walivyofanya pia.
Jambo la tatu ambalo Mhe Rais
Dkt Magufuli amelionyesha ni kule kutoa wito kwa chama chake cha CCM ambapo
yeye ndiye mwenyekiti wake kwamba sekretarieti husika iwasilishe ripoti juu ya
viongozi wana-CCM wanaotajwatajwa katika kashfa za kila mara ilichama
kiwashughulikie.
![]() |
Ikulu jijini Dar es Salaam |
Rais amesema chama kinazo
taratibu zake za kuwaadhibu wanaojihusisha katika kashfa kadha wa kadhaa. Nyakati
zingine si kawaida sana kuwaeleza wana-CCM wenzake mbele ya umma bali hufanyika
vikao vya ndani ya chama na ndiko wanakoelezana haya.
Hii inadhihirisha wazi Mhe
Rais ameanza kuchoka kuwavumilia wana-CCM wenzake hadi kulazimika kuitisha
chama kilete ripoti hiyona kujadiliwa kama dondoo maalum ya mkutano.
Jambo la nne alilolionyesha
Mhe Rais ni kule kukiri wazi kwamba wateule wake
wanamwangusha na wajumbe wa kamati hiyo ya bunge imemwonyesha imani kubwa kwamba
wanaweza kumsaidia vizuri katika uongozi wa nchi kwani wameonyesha
uzalendo wa hali ya juu sana.
Rais amesema wazi kwamba,
baada ya kupokea ripoti ya kamati hii ya bunge, sasa amepata wasaa wa kuangalia
upya timu ya watendaji wake watakaomsaidia kuendesha serekali, huenda
akalazimika kufumua baraza zima lamawaziri na kuliunda upya na kuwateua baadhi
ya wabunge kumsaidia.
Ni wazi Mhe Rais ameonekana
kufarijika sana kwa kazi nzuri iliyofanywa na Spika wa bunge kwa kushirikiana
na wabunge wote.
Rais pia ameonyesha
kuridhika sana na ripoti mbili hizi zilivyoandaliwa kwani zilipitia mtindo wa
mikataba ya madini, inavyosafirishwa nje ya nchi na mapato au kodi inayolipwa
serekalini.
Hongera sana Rais pamoja na
Waziri Mkuu wako. Hongera pia Mhe Spika na wabunge wote kwa uzalendo mkubwa.
Watanzania sasa tuipe
serekali nafasi ili kazi iliyoelekezwa kwa TAKUKURU ifanyike vizuri na kuikamilisha
mapema kama alivyo elekeza Mhe Rais Magufuli.
“MUNGU
IBARIKI TANZANIA”.
No comments:
Post a Comment