SERIKALI
imewashauri wadau wote wa mambo ya habari hapa nchini kujenga umoja ili
kuisaidia utekelezaji wa sheria mpya ya huduma za habari ya mwaka 2016 iweze kutumika.
Akiongea na wadau wa habari
mjini Dodoma katika warsha ya siku moja iliyowashirikisha serikali na wadau wa
habari nchini, Naibu Waziri wa Habri, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Mhe Annastazia
Wambura aliwaeleza washiriki katika warsha hiyo umuhimu wa kuwa kitu kimoja.
Naibu Waziri alisema, “ili
kuisaidia serikali kufanyia kazi baadhi ya mambo yanayoonekana kuleta ukakasi
katika sheria ya huduma ya habari ya mwaka 2016, ni vizuri wadau wote tukawa na
umoja, ili kusaidia ufanisi wa sheria hii,alieleza Naibu Waziri.
Naibu Waziri wa Habri,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe Annastazia Wambura akiwahutubia wadau wa Habari (hawapo pichani) katika warsha ya MISA mjini Dodoma jana.
Alieleza pia kwamba, serikali
inayo nia njema ya kupitisha sheria hii,
ili kuboresha sekta ya habari hivyo wadau wasiione serikali kama adui kwao,bali
ni kulenga kusaidia mfumomzuri wa kusimamia mambo ya habari hapa nchini
kulingana na wakati uliopo,alifafanua Naibu Waziri.
Wakati huo huo, Naibu
Waziri Mhe Wambura aliwataka wadu wa habari kujikita zaidi katika kuzingatia
maadili na miiko ya uandishi wa habari na kamwe wasitumie kalamu zao kupotosha umma bali
wazingatie ukweli.
Naibu Waziri alitolea
maelezo kwa kurejea mchango wa maoni uliotolewa katika warsha hiyo na Mbunge wa
Jimbo la Mpanda Vijijini, Mhe Moshi
Seleman Kakoso kwamba, wadau wa habari wanakiuka maadili ya uandishi kwa kutokuwa
wakweli kwa kubinya kimaudhui kwa taarifa wanazo toa.
Katika marejeo hayo Naibu
Waziri alieleza wito wa Mhe Kakoso kwamba, “kuna tatizo la ukiukaji mkubwa wa
kimaadili kwa baadhi ya waandishi na vyombo vya habari kwa kuweka kichwa cha
habari kikubwa juu ya kurasa wa mbele wa gazeti, lakini ukienda kwa undani
katika habari hiyo, hupati maelezo husika kwa kina hivyo kubinya maudhui ya
taarifa hiyo na kuacha maswali mengi kwa msomaji.
Naibu Waziri alitoa wito kwamba
ni vizuri wadau kuzingatia maadili ya kiuandishi ili kuzuia makali ya sheria hii
mpya isije kuwagusa na kuilamu serikali
kwamba haina malengo mazuri na vyombo vya habari.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Idara
ya Habari-Maelezo, Bi Zamaradi Kawawa aliwaeleza washiriki wa warsha hiyo kwamba,
wadau wa habari wakiwamo wamiliki wa vyombo vya habari, wahariri na waandishi
waipe muda sheria mpya ya huduma ya habari ya mwaka 2016 ianze kutumika kwanza,
kuliko kuanza kuilalamikia ingali bado mapema.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo Bi Zamaradi Kawawa akiwahutubia wadau wa Habari katika warsha ya MISA mjini Dodoma jana. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Habri Mhe Annastazia Wambura na wadu wengine.
Kaimu Mkurugenzi huyo
alieleza pia kwamba, ikiwa itabainika upo ugumu wa baadhi ya maeneo katika
sheria hiyo basi Idara pamoja na wadau wa Habari watakaa pamoja ili kutoa mapendekezo
kwa vyombo husika vya serikali ili kuipitia na kurekebisha.
Warsha hiyo ya siku moja
iliandaliwa na Wizara ya Habari kushirikiana na MISA ili kujadili njia nzuri
zaidi ya kujenga mahusiano ya kiutendaji baina ya serikali na vyombo vya habari
hapa nchini.
Naibu Waziri Mhe Annastazia Wambura katika picha ya pamoja na wadau wa Habari mjini Dodoma jana.
Washiriki katika warsha
hiyo walikuwa wamiliki wa vyombo vya habari, wahariri, waandishi, viongozi wa
MISA, TMF pamoja maafisa habari wa baadhi ya Idara za serikali, wabunge na
wanasheria.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment