WAZIRI
wa
zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa sasa wa Sengerema (CCM), Mhe William
Ngeleja amerejesha serikalini fedha za mgao wa Escrow Tshs 40.4 milioni hivi
leo.
Kulingana na taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya Habari leo jijini Dar es Salaam, Mhe Ngeleja amesema
ameamua kufanya hivyo ili kulinda hadhi na heshima yake kwenye jamii.
Suala la fedha za akauti ya
Escrow ni moja ya mambo ambayo serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa
Rais Dkt John Pombe Magufuli imeamua kupambana nayo na hadi sasa wamiliki wa
Kamapuni ya Ufuaji Umeme ya IPTL ya Dar es Salaam ambao ni Harbinder Sethi
Singh na James Rugamalira tayari wapo kizuizuini kwa tuhuma hiyo.
Taarifa hiyo imeeleza pia
kwamba, mnamo February 12, 2014 Bwana James Rugemalira ambae ni mmiliki wa
kamapuni ya VIP Engineering and Marketing Ltd alimpatia kiasi hicho Waziri huyo
wa zamani fedha hizo kupitia benki ya Mkombozi ya jijini Dar es Salaam.
Ameeleza madhumuni ya fedha
hizo ilikuwa zimsaidie kutekeleza majukumu yake ya kibunge kwenye jamii
anayoiongoza yaani wananchi wa Jimbo la Sengerema bila kujua zilikuwa na harufu
ya tuhuma za rushwa.
Pia, Mhe Ngeleja amesema katikataarifa
yake kwamba ni jambo la kawaida wabunge kuomba misaada toka kwa wahisani mbalimbali
wa ndani na nje ili kujipatia fedha za kusaidia mipango ya kijamii ambayo
bajeti ya serikali haiweza kuijumuisha mfano ujenzi wa makanisa, misikiti na
kusaidia malipo ya ada kwa wanafunzi wasio na wazazi au walezi.
Hata hivyo, taarifa hiyo
ilisema kwamba Mhe Ngeleja mnamo January 15, 2015 alilipia kama kodi kwa aijili
ya pato la fedha hizo kwa kiwango cha
asilimia 30% ilivyo sheria kwa Mamlaka
wa Mapato nchini yaani TRA, amabpo alilipiakiasi cha Tshs 13.138 milioni, taarifa
hiyo ilisema.
Tuhuma za wahusika wa
akaunti ya Escrow kwa sasa wanatakiwa na vyombo vya serikali kutoa ushirikiano ili
kuona jinsi walivyozipata fedha hizo na ikiwa wana hatia ama lah.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment