PROFESA JAY: AITEKA DAR ES SALAAM. - Mazengo360

Sunday, 9 July 2017

PROFESA JAY: AITEKA DAR ES SALAAM.

“Upo usemi; wote wenye hofu ya Mungu hufanikiwa.”

Prof+J+PX+1


Ni kama weekend hii jiji la Dar es Salaam lilitekwa kwa muda na mbabe wa muziki wa hip pop nchini, Joseph Haule ambae pia ni Mbunge wa Mikumi (CHADEMA).

Profesa Jay, alifunga ndoa na mchumba wake Grace waliochumbiana kwa muda mrefu takribani miaka 13, kama vile alivyofanya mchezaji wa Barceloan, Messi amabe pia majuzi alifanya kama Profesa Jay, walipofunga pingu za maisha pale kanisa la Kuu la Cathedrali la Mt Joseph la Jimbo Kuu la Dar es Salaam hapo jana.

Kama haikutosha, wakaamia ukumbi wa Mlimani City, baada ya kubebwa na magari ya kijanja ya tena ya kisasa aina ya Range Rover mapyaaa na upya wake.

Huku akisindikizwa na wapambe wake wabunge wa Ukawa, mijeda yote nguli tena wa nguvu akina Peter Mhe Msigwa, Mhe Joseph Mbilinyi aka Sugu, na kiboko cha mzee wa Kiraracha, Mhe Mbunge Mbatia nao walikuwepo.

Sasa kule Mlimani City usipime.

Prof+J+PX+2


 DJ Mkuu na kiongozi wa CHADEMA aka mhangawa uwekezaji Mhe Freeman Mbowe nae akatia timu akiwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mhe Mzee Lowasa ilivyo jadi yao.

Lilikuwa bonge la movie, pale ambapo mfalme wa muziki wa kizazihiki hapa nchini, Diamond Plantinum alipofanya vitu vyake live pale stajini Mlimani City, huku Mzee Lowasa, M/k wa CHADEMA Mhe Mbowe na Mbunge Mbatia wakishuhudia kama majaji.

Inavyooneka Diamond pia alitambulisha mtindo mpya wa uvaaji kwa vijana wa leowa jinsi ya kiume, ambapo mtindo wa suruali aina ya “don't touch” au “mchinjo” umerudi rasmi sokoni.

Diamond akipigilia “kobazi” (open shoes) zake za kijanja akaonekana simple, ambapopia aliungwa mkono pale stajini na mkali wingine anaetamba hivi sasa, Harmorraper nae alitinga na “don't touch” yake kimtindo.

Akina dada wa kibongo nao hawakubaki nyuma pamoja na vijana walipagawa na simu zao, huku wakigombania kupata picha za kuuza sura na mfalme huyo wa muziki hapa nchini Diamond Plantinum.

Professa Jay, nae hakubaki nyuma.
Alijimwaga stajini kucheza ngoma mpya ya Diamond akiwa na mahabuba wake Grace, huku akishikilia mkia wa gauni lake lisiburuze chini la rangi ya dhahabu ya kung’aa.

Katika dansi hilo kakaaa, zilipigwa ngoma za kijanja toka majuu zilizobamba miaka ya nyuma.

 DJ Mkuu Mhe Mbowe, pamoja na kijana wa Arusha mjini Mhe Mbunge Lema na mkewe, pamoja na Mhe Mbatia pia na mkewe waliyarudi kisawasawa mangoma ya kijanja na kuendana kabisa na mdundo unayopigwa zaidi kule Uingereza katika Ukumbi wa Etihad pale Machester City. 

Wakali hawa walinikumbusha enzi zetu miaka ya 80 na 90 tulipokuwa tukisoma shule za bodini za sekondari, enzi hizo kwa hela yakahawa miziki hiyo tuliicheza sana hadi tulikuwa tukitoroka shule na kwenda kwenye muziki.

Kipindi hicho shule za Kibohehe, Mawenzi, Namfua, Kilimanjaro na zingine za mkoani Kilimnjaro miaka hiyo, wacha kabisa.

Kiukweli weekend hii Professa Jay na mkewe Grace ndio habari ya mjini.

Nahisi bajeti nzima ya harusi hiyo sijui ilikuwa kiasi gani,kwani sijaona popote mambo yalifanyika kishamba,hata kidogo.

TUNA WATAKIA WAWILI HAO, JOSEPH NA GRACE MAISHA MEMA NA YENYE BARAKA TELE. MUNGU IBARIKI NDOA YAO.

MWISHO.