ASHAURI WATANZANIA KUHESHIMU MUDA. - Mazengo360

Monday, 10 July 2017

ASHAURI WATANZANIA KUHESHIMU MUDA.


Pousen+3

MTANZANIA anaecheza soka ligi ya Ujermani katika klabu ya RB Leipzing, Yussuf Poulsen ameshauri watazania waheshimu thamani ya muda kama wanataka kufikia maendeleo wanayo yatamani.
Yussuf mwenye umri wa miaka 23 na mwenye asili ya baba ambae ni mtazania kutokea jijini Tanga na kuzaliwa na mama mwenye asili ya Denmark, ameitembelea Tanzania hivi karibuni na kuhojiwa na mtandao wa kijamii wa Ayo Tv na kutoa ushauri huo.
Mtandao huo wa Ayo Tv ulimfanyia mahojiano maalum mtazania huyo, ikiwamo sababu za kuchezea soka lake kama mchezaji wa timu ya Taifa ya Denmark badala ya timu ya Taifa ya Tanzania, alisema hajawahi kuombwa kufanya hivyo na vyombo husika toka Tanzania.

Pousen+4

Alipoulizwa ni jambo gani baada ya kufika nchini lililo mshangaza sana na pia ni kitu gani anachoshauri wachezaji wa kitanzania ili waweze kufikia mafanikio kama aliyonayo hivi sasa, Yussuf alieleza kwamba,
“Ninashangazwa sana jinsi watanzania wasivyo zingatia thamani ya muda,” alieleza mshambuliaji huyo wa RB Leipzing ya Ujermani na mchezaji wa timu ya Taifa ya Denmark.
Alitoa mfano wa wazi kwamba, mtu anaweza kupokea mwaliko wa kukutana na mtu mwingine au hata kufanya mahojiano na mtu mwingine kwa muda fulani waliokubaliana, lakini cha kushangaza muhusika badala ya kufika eneo husika nusu saa au robo saa kabla ili kuwahi muda, yeye hufika nusu saa au saa moja baadae, kitu alichoeleza kwamba sio kujali thamani ya muda.
Yussuf alitoa mfano toka nchini Ujermani na Denmark kwamba suala la kuzingatia muda ni jambo la kisheria na pia linachukuliwa kama ni jadi ambapo yeyote anaechezea muda au kutozingatia muda, huweza kuchukuliwa hatua za kisheria.

Pousen+2

Amewataka watanzania kuzingatia zaidi thamani ya muda na pia ametoa ushauri kwa wachezaji wa kitanzania kujitoa sadaka na kuachana na mambo mengine na kufanya jitihada na bidii zaidi kama wanataka kufikia mafanikio.
“Wachezaji wa kitanzania ni vyema mkazingatia suala la muda na pia mjitoe sadaka kutumikia soka, endapo mnataka kufikia mafanikio,” alishauri zaidi Yussuf.
(Taarifa na picha kwa hisani ya Millard Ayo Tv na mitandao wa wikipedia) .

MWISHO.