WAFUNGAJI WAKUTANA DODOMA KUJADILI UCHUMI WA VIWANDA. - Mazengo360

Thursday, 13 July 2017

WAFUNGAJI WAKUTANA DODOMA KUJADILI UCHUMI WA VIWANDA.

CHAMA cha wafugaji nchini (CCWT) wamekutana mjini Dodoma hapo jana kujadili namna ya kubadilisha ufugaji wao ili uendane na sera ya Rais Dkt John Pombe Magufuli ya uchumi wa viwanda.
Akitoa taarifa ya mkutano huo mbele ya waandishi wa habari, mratibu wa mkutano huo ambae pia ni Katibu wa Chama hicho Kanda ya Kati Bi Neema Ally alisema lengo kuu ni kujadili na kutathmini ushauri wa Mhe Makamu wa Rais Bi Samia Suluhu Hassan alioutoa kwa wafugaji alipokuwa mjini Arusha mwezi uliopita juu yaufugaji unaoendana na sera ya serikali ya uchumi wa viwanda.
Pia, alieleza kwamba kulingana na hotuba aliyoitoa Mhe Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akihairisha Bunge jumalililopita mjini Dodoma, aliwashauri wafugaji kuandaa mpango wa ufugaji wenye tija ili serikali iweze kuwasaidia kuwapatiamaeneo ya malisho na mipango mingine.
Mkutano huo uliwakilishwa na wenyeviti wa kanda wa wilaya na Kanda zote saba hapa nchini, ikiwamo Kanda ya Kati yenye mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida, Kanda ya Ziwa yenye mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Mara na Geita.
Kanda zingine ni ya Magharabi yenye mikoa ya Tabora, Kigoma, Katavi na Bukoba na Kanda ya Mashariki ambayo ni Dar Es Salaam, Pwani, Mtwara, na Lindi.
Alitaja pia Kanda zilizohudhuria ikiwamo Kanda Kaskazini yenye  mikoa ya Tanga, Kilimanajoro, Arusha na Manyara pamoja na ile ya Nyanda za juu Kusini ya mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya na  Sumbawanga.
Akitoa mada katika mkutano huo, mwakilishi toka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, ambae pia ni Afisa Mifugo Mkuu wa Wizara, Bwana Simon Lyimo aliwaambia wafugaji hao kwamba, ni vizuri kutambua mabadiliko ya tabia nchi yanavyoathiri ufugaji na kuwataka wabadilike.
Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya “Tanzania Livestock Product Ltd, Ernest Tarimo inayojishughulisha na uongezaji thamani ya bidhaa zitokanazo na mifugo zikiwamo nyama, maziwa na ngozi aliwashauri wafugaji hao juu ya kuunda mfumo madhubuti wa uongozi ili hoja yao ya kutaka kuanzisha kamapuni ya kusindika nyama nchini iweze kufanyiwa kazi na serikalikwa urahisi zaidi.

Wafugaji+1
Katibu wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT)  Bwana Magembe Makoe akisoma mapaazio ya kikao mbele ya washiriki (hawapo pichani) katika mkutano wa wafugaji iliofanyika Dodoma hapo jana.

Alieleza zaidi Mkurugenzi huyo kwamba, ili wafugaji waendane na sera ya serikali ya ujenzi wa viwanda, wafugaji lazima wajadili njia ya kupata mtaji wa shilingi bilioni 50, unaotakiwa katika mapendekezo ya kuanzisha kampuni ya kusindika nyama na mazao mengine ya mifugo kwa njia ya uuzaji wa hisa.
Amewataka pia waachane na ufugaji wa kizamani kwani malisho kwa sasa ni shida na pia wasibakie kupishana na serikali kugombania malisho na badala yake watumie ushauri wa wataalam katika kufanya ufugaji bora na wenye tija.

Wafugaji+2
Washiriki ambao ni wafugaji toka maeneo mbalimbali nchini wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano wa wafugaji uliofanyika mjini Dodoma kujadili uchumi wa viwanda hapo jana.

Mkutano huo wa siku moja ulipitia na kupitia pia maazimio ya taarifa ya wafugaji itakayowasilishwa kwa majadiliano ya pamoja kati ya uongozi wa CCWT na ofisi ya Waziri Mkuu baadae mwezi huu, kufuatia hoja ya Mhe Kassim Majaliwa alivyowashauri.
MWISHO.