KUMBUKUMBU KIFO CHA PRINCESS DIANAH USIPIME. - Mazengo360

Saturday, 8 July 2017

KUMBUKUMBU KIFO CHA PRINCESS DIANAH USIPIME.

WATOTO wawili wa uzao wa mkwewe Malkia wa Uingereza, Princess Dianah aliyefariki August 31, 1997 wamedhamiria kumuenzi ipasavyo mama yao baadae mwezi ujao kwa kutimiza miaka 20 tangu kifo hicho.
Kulingana na maelezo ya gazeti leo la Uingereza la “The Dailymail” limeeleza, watoto hao ambao ni Prince William na Prince Harry watafanya hivyo baadae mwezi ujao kwa kuandaa kipindi maalum cha mahojiano ya Television ya ITV ya Uingereza.

Princess+Dianae+with+her+two+sons
Princess Dianah akiwa na wanae kabla ya kifa chake August 31, 1997

Prince Harry amesema kwamba, hii ni mara ya kwanza kwa wao wawili kufanya hivyo tangu mama yao alipofariki mnamo August 31, 1997.
Ameeleza pia kwamba, kutokana na hali ya ujana uliokuwa ukiwakabili vijana hao hapo mwanzo, hawakuona umuhimu wa kufanya hivyo mapema, lakini kwa sasa wamekuwa watu wazima hivyo wametambua umuhimu wa kumuenzi mama yao inavyo stahili.

Prince+Harry%252C32%252C
Prince Harry, kwa sasa umri wa miaka 32.

Pia amesema kwamba, wanatambua mama yao alikuwa mama bora kwao na tena mwenye mapenzi ya dhati kwao kushinda vitu vyote duniani, hivyo na wao wata muenzi ipasavyo”, alifafanua Prince Harry.
Amemalizia kwa kusema zaidi kwamba, katika mahojiano hayo na Television ya ITV ya kwamba, wataonyesha kwa uwazi mahusiano yaliyopo kati yao na mama yao Princess Dianah na pia wataelezea hisia zao zinavyoguswa na historia ya mama yao.

Prince+William
Prince William.

Pincess Dianah alikuwa kipenzi cha watu, hususani alivyo jihusisha na masuala ya kijamii ikiwamo tasnia ya urembo na kugusa mioyo ya watu wengi.
Wakati wa kifo chake alimwacha Prince Harry akiwa naumri wa miaka 12 tuu, kifo kilichoamsha hisia kubwa kwa watu hadi leo, ingali bado anaishi katika mioyo ya watu wengi.

MWISHO.