MJUE DR KLERUU: NYOTA ILIYO POTEA. - Mazengo360

Saturday, 8 July 2017

MJUE DR KLERUU: NYOTA ILIYO POTEA.

Dr+Kleruu+Peuget

ILIKUWA siku ya sikuku ya Noel au Christmas mnamo mwaka 1971. Mkuu mpya wa Mkoa wa IRINGA aliye hamishiwa hapo akitokea Mtwara Dr. Wilbert Kleruu, msomi wa shahada ya uzamivu wa uchumi wa kijamaa katika kilimo. 

Kipindi hicho Kulikuwa na kampeni ya kutaifisha mashamba ya wakulima wakubwa na kuyafanya mashamba ya kijiji. Na Dr Kleruu alipelekwa Iringa ili akatekeleze kaz hiyo  kwani kipindi hicho iringa ilikuwa na wafanya biashara wakubwa walio miliki mashamba makubwa ya kilimo hasa maeneo ya Isimani. 

Katika Eneo hilo la Isimani Kulikuwa na mkulima mmoja aliye kuwa ana miliki Takribani hekari 400 za mashamba na mfanyabiashara aliye kuwa ana miliki majumba iringa mjini - Said Mwamwindi.  
Kwa wakati, ule ilishauriwa angalau kila mtu awe na shamba lisilo zidi hekari 4. Jambo ambalo lilileta mvutano Mkubwa kati ya wakulima wakubwa na Serikali. 

Sasa siku hiyo ya Christmas Dr. Kleruu alikwenda Isimani akiwa katika utekelezaji wa sera ya kutaifisha mashamba.  Moja kwa moja alikwenda hadi shambani kwa Mwamwindi, na kumkuta analima. 

Mkuu wa Mkoa akamuuliza mbona unalima shamba lako mwenyewe na si la kijiji? Mwamwindi akajibu, sioni tatizo hakuna mtu shamba ni, Leo ni jumapli tena ni sikuku

Maneno Yale yalimuudhi Dr Kleruu, ambaye alikuwa akisifika kwa ukali, kutekeleza sera za serikali, na maneno makali au kutukana watu hadharani pale wanapo fanya makosa. 

Dr. Kleruu baada ya kuudhika alimtukana Mwamwindi tusi lililo mlenga mama yake ambaye tayari alikuwa amesha kufariki siku nyingi. 

Mwamwindi alihoji inakuwaje ana mtukania mama yake, huku akimuonyesha kaburi alimo zikwa. 

Mkuu wa Mkoa, aliendelea kuja juu, huku akisema kaburi ndio nini? Huku akilipiga mateke kaburi la Mama yake Mwamwindi. 

Na ifahamike kwa kabila la wahehe makaburini yana heshima yake, Kwani ndipo nyakati nyingine hutumika katika Sala, matambiko na mila kadha,. 

Kitendo kile kilimgadhabisha Mwamwindi, na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani.  Mkuu wa Mkoa akadhani Mwamwindi ana mkimbia, akaamua kumfuata hadi nyumbani. 

Alipo fika nyumbani, tayari Mwamwindi alisha ingia ndani na kuchukua bunduki yake, Dr. Kleruu baada ya kuona hali ile mara moja alianza kumuomba msamaha, Lakini hasira  zilimuwaka Mwamwindi kama moto wa nyika, hakuwa na msamaha, alimfyetulia risasi Dr Kleruu na kumuua

Baada ya kumuua, Mwamwindi aliuchukua mwili ya Mkuu w mkoa na kuuweka ndani y gari (seat ya nyuma) alilo kuja nalo Mkuu huyo wa Mkoa, gari aina ya Peugeot. 

Baada ya hapo alichukua kofia ya Dr Kleruu na kuivaa, kisha akiingia ndani ya gari na kuanza safari ya kuelekea iringa mjini. Tena akipita njia isiyo ruhusiwa kwani barabara ilikuwa 'one way'

Alipo karibia mjini, Askari walishangaa ni nani anaye pita njia isiyo ruhusiwa, ila mara waligundua ilikuwa gari y RC wa iringa, hivyo walidhani amepata dharura. 

Gari ilipo wasilini kituoni, polisi walijiandaa kupiga salute, mara alishuka Mwamwindi akiwa na bunduki yake na kuelekea ndani (counter). Askari walipigwa na butwaa. 

Alipo fika aliwaambia "nendeni mkachukue Nguruwe wenu ndani y gari," na Kisha akakabidhi bunduki yake.

Lilikuwa tukio la kuajabisha, na kushangaza na lililo fanyika kwa haraka sana. 

Baada ya taarifa kuenea, msako wa polisi ulianza mara moja. Msiba wa Dr. Kleruu ulikuwa pigo kwa wakulima wadogo,walio sikitika kwa kifo hicho. 

Ila katika msako huo, polisi waliwakamata baadhi ya watu walio kuwa wakinywa bia kwa furaha, shangwe  na nderemo baada ya kusikia Dr Kleruu ameuawa.  Kwani wanadai alikuwa na dharau,. 

Kesi ya Mwamwindi alipelekwa haraka sana,. Na ndani ya miezi kadhaa, June 1972, Mwamwindi alihukumiwa kunyongwa hadi kufa, ikiwa ni moja ya hukumu chache za kunyongwa zilizo wahi kuidhinishwa. Huo ndio ukawa mwisho wa tajiri na mkulima mkubwa, Saidi Mwamwindi. 

Mwisho.