MCHEZAJI WA MANCHESTER UNITED AWA PADRE. - Mazengo360

Thursday, 13 July 2017

MCHEZAJI WA MANCHESTER UNITED AWA PADRE.

PHILIP MULRYNE ambae alikuwa mcheza soko katika club ya Manchester United ya Uingereza ambae aliichezea ligi ya Premier hapo siku za nyuma ametawazwa kuwa Padre wa madhehebu ya Kikatoliki huko Ireland.

Philip+Mulyren+1
Padre Philip Mulryne akiwekewa mikono na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dublin Joseph Augustine Di Moia huko Ireland juma lililopita na kuwa kasisi (Padre) wa Kikatoliki rasmi.


Mcheza soka huyo, mnamo tarehe Julai 08, 2017 alitunukiwa wadhifa huo kwa mamlaka ya sheria za Kanisa Katoliki Dunia huko Northern Ireland chini ya Shirika la Wadomisiani (Domician Order).

Mwanasoka huyo ambae kwa sasa anajulikana kwa cheo cha Father Mulryne, inaripotiwa  alikuwa akilipwa kitita cha Euro 600,000 kwa mwaka wakati akiichezea Manchester United ya Uingereza.

Philip+Mulyren+3
Padre Philip Mulryne kabla ya kufikia kusimikwa rasmi kuwa kasisi (Padre) akiwa amelala chini kuonyesha utii na unyenyekevu wakati sala kuu ya masifu ya watakatifu (Litania kulingana na madhehebu hayo) ikisomwa.

Father Mulryne amepewa daraja hilo la upadre na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dublin Joseph Augustine Di Moia ambaye alisafiri kutoka Roma kwa ajili hiyo.

 Father Mulryne aliweka nadhiri za kuishi maisha ya kitawa na kutunukiwa pia  daraja la Ushemasi kulingana na taratibu za kanisa Katoliki mnamo Oktoba mwaka jana 2016.  

Katika maisha yake ya ujana katika michezo, Father Mulryne  alifanikiwa kujiunga na timu ya Manchester United mwaka 1997 baada ya kuonesha kipaji katika timu za vijana na pia kuichezea timu ya Taifa ya Northern Ireland.

Philip+Mulyren+2
Padre Philip Mulryne enzi zake akisakata soka katika timu yake ya Taifa ya Ireland.

Aliachana na Soka rasmi mwaka 2009 na akaanza safari yake ya kuelekea wito wa upadre na akajiunga na malezi ya Seminari ilivyo desturi. 

Miaka miwili alisoma masomo ya Falsafa katika Chuo cha Queen's University cha Belfast na Maryvale Institute kabla ya kujiunga na masomo ya Theolojia katika Chuo cha Pontifical Irish College na baade Chuo Kikuu cha Gregorian huko Italia.

Kulingana na taratibu za Kanisa Katoliki, hua linautaratibu wa kuwapata vijana wenye vipaji mbalimbali vya hali ya juu kadiri walivyozaliwa navyo ili waweze kusaidia jamii kubadilika na kuishi maisha mema wakati wa utumishi wao katika jamii.

(Taarifa hii na picha kwa hisani ya BBC)

MWISHO.