WENGINE KUSIMAMISHWA AJIRA MWEZI HUU. - Mazengo360

Thursday, 13 July 2017

WENGINE KUSIMAMISHWA AJIRA MWEZI HUU.


PS-Utumishi
Katibu Mkuu Utumishi Dkt Laurian Ndumbaro.

WIZARA ya Utumishi wa Umma leo imetoa waraka mpya kuhusu wale ambao hawajawasilisha vyeti vya kuhitimu kidato cha Nne na Sita ili vihakikiwe na baraza la mitihani laTaifa wasimamishiwe mishahara yao kunzia mwezi huu wa July.
Kulingana na waraka uliotolewa hivi punde leo jioni toka Ofisi ya Katibu Mkuu Utumishi mjini Dodoma kwenda kwenye vyombo vya habari, umewaagiza waajiri wote nchini katika sekta ya umma nchini, kutekeleza mara moja agizo hilo.
Waraka huo umeeleza bayana juu ya mwongozo wa waraka wa serikali kwa watumishi wa umma no. 1 wa mwaka 2004, ambapo ulieleza utaratibu wa ajira serikali na kutaja kiwango cha chini cha elimu ni kidato cha nne.
Kwa maelekezo haya yakusimamisha mishahara ya wale wote ambao vyeti havijawasilishwa kwa uhakiki, ina maana kusimamishwa ajira hadi hapo taarifa zao zitakapothibitishwa kuwa zipo sahihi.

MWISHO.