RAIS MSTAAFU WA IRELAND ALIPONGEZA BUNGE LA TANZANIA. - Mazengo360

Friday, 14 July 2017

RAIS MSTAAFU WA IRELAND ALIPONGEZA BUNGE LA TANZANIA.

ZIARA ya Rais Mstaafu wa Ireland pamoja na mwenziwe Graca Machel  wamelipongeza Bunge la Tanzania kwa kufanya jitihada za kutosha kutunga sheria zinazo lenga kutunza afya ya jamii wakiwamo wazee, akina mama na watoto.

Speaker+3
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe Job Ndugai (kulia) akimkabidhi Rais Mstaafu wa Ireland Bi Mary Robson picha ya jengo la ofisi ya Bunge ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma hapo jana.

Ugeni huo uliomtembelea Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai ofisini kwake hapo jana mjini Dodoma, walieleza jinsi walifurahishwa na hatua serikali ya Tanzania ilizofikia pamoja na Bunge la Tanzania wanavyo shirikiana kutekeleza malengo ya Umoja wa Mataifa kuhusu afya ya jamii, japo zipo changamoto.
Rais huyo mstaafu wa Ireland Bi Mary Robson na Bi Graca Machel kwa nyakati tofauti wakati wa mazungumzo yao na Spika, walieleza jinsi walivyofurahishwa na ziara yao hapa nchini na kuzuri pia mkoa wa Dodoma ikiwamo wilaya ya Bahi na kusema wameridhishwa na jitihada zilizoonyeshwa.

Speaker+1
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akimsikiliza Bi Graca Machel kwa makini hapo jana baada ya ugeni huo kumtembelea ofisini kwake. Katikati ni Rais Mstaafu wa Ireland Bi Mary Robson.

Bi Graca Machel yeye alisema, malengo ya ziara hiyo ni kujionea jinsi serikali ya Tanzania na vyombo vyake ikiwamo Bunge inavyotekeleza utoaji huduma kwa wazee, ambapo wao ni wadau wakubwa katikampango huo hususani afya za wazee.
Bi Graca Machel alimshauri Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai na Bunge pamoja na serekali kwa ujumla, wasiridhike na hatua iliyofikiwa hadi sasa bali waendelee na jitihada hususani katika kutunga sheria zitakazowezesha mazingira rafiki yakayotoa fursa zaidi katika kutoa huduma ya afya kwa akina mama, watoto na wazee.

Speaker+2
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akiagana na ugeni wake Bi Mary Robson (katikati) na Bi Graca Machel kwenye lango kuu la ofisi ya Bunge mjini Dodoma hapo jana, baada ya kumtembela Spika na kufanya nae mazungumzo.

Nae Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai alipokea salamu hizo za pongezi toka kwa viongozi hao na kuahidi kuendelea kuandaa sheria zenye kuleta mafanikio zaidi katika sekta ya afya hapa nchini.

MWISHO.