TANZANIA NA MAAJABU YA MUNGU. - Mazengo360

Friday, 14 July 2017

TANZANIA NA MAAJABU YA MUNGU.

Lion+3

TANZANIA inaingia tena kwenye vitabu vya historia na maajabu, baada ya kwenye moja ya mbuga za utalii nchini kuonekana  Simba akimyonyesha mwana chui.

Wawili hao walikutwa na mtalii Joop Van Der Linde mgeni katika eneo la utalii la Ndutu Safari Lodge hapa nchini katika eneo la uhifadhi la wanyama pori huko Ngorongoro.

Lion+1

Limekuwa tukio la ajabu kwa sababu ya utofauti wa jamii ya wanyama hawa, Simba akitokea jamii ya Leo na Chui akitokea jamii ya Tigris. Wote wakiwa ni Panthera.

Eneo hilo ni la ukanda wa Serengeti ambapo Simba huyo amepewa jina Nosikitok na ana umri wa miaka mitano.

Lion+2

Wahifadhikatika porihilo amewekewa Simba huyo mfumo wa GPS katika shingo yake ili kufuatiliakwa karibu zaidi tabia zake.

Kwa msaada wa  chombo hicho Simba huyo amegundulika kuwa na watoto watatu waliozaliwa kati ya mwezi Juni 27-28, mwaka huu.

(Chanzo: BBC SWAHILI na Picha kwa hisani ya Joop Van Der Linde/ Ndutu Safari Lodge).

MWISHO.