SEREKALI YAPONGEZA MCHANGO WA UN-HABITANT. - Mazengo360

Tuesday, 18 July 2017

SEREKALI YAPONGEZA MCHANGO WA UN-HABITANT.

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh Selemani  Jafo(Mb) amelipongeza Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa(UN-Habitat) kwa kuanzisha ushirikiano na Serikali kwa kuweka mpango wa kuboresha Miji endelevu Mkoa wa Dodoma.

Jafo+2
Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe Seleman Jafo.

Mhe Jafo aliyasema hayo mjini Dodoma mwishoni mwa juma lililopita alipokuwa akifunga warsha iliyowashirikisha waataalam wa makazi toka Shirika la Umoja wa Taifa na Mamlaka ya mafunzo ya Ufundi nchini (VETA) kupitia wizara ya TAMISEMI.

Mhe.Seleman Jafo amewataka wataalam  kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI kushirikiana kikamilifu na wadau mbalimbali ambao wanataka kuleta maendeleo mjini Dodoma kwa kuwa serikali ya sasa inahitaji mpango shirikishi kwa wataalam wetu na kwa wananchi kwa ujumla.

Mhe Jafo alitoa wito kwa watendaji katika sekta inayojishughulisha na ustawishaji wa miji na makazi kutilia umuhimu wa kupanga vizuri miji midogo hususani ile inayozunguka mji wa Dodoma baada ya serekali kuhamishia shughuli zake toka Dar kuja Dodoma, ili iwe kivutio cha utalii na biashara hapo baadae.

Jafo+1
Naibu Waziri wa TAMISEMI (katikati) Mhe Seleman Jafo akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa UN-HABITANT na wawakilishi wa Mamlaka ya mafunzo ya Ufindi VETA,mjini Dodoma mwishoni mwa juma lililopita.

Ameshauri miji yote inayozunguka mkoa wa Dodoma ni vizuri ikafanyiwe tathmini nzuri na ipangwe kwa lengo la kuvutia utalii na si kuiacha ikue kihole kama inavyofanyika hivi sasa, alisema.

“Miji midogo iliyopo pembezoni mwa mkoa wa Dodoma inakuwa  kwa mfano Chemba, Bahi, Kibaigwa ambayo inakuwa pasipo kuwa na mpangilio mzuri ni wakati wa wataalam waliopata mafunzo haya kutoa ushirikiano katika kuboresha makazi yao ili yawe ya kisasa na endelevu na kuwa kivutio kwa wageni wanaokuja” alisema Mhe Jafo.

Mhe Jafo ameongeza kwa kusema “anaishukuru taasisi ya UN HABITAT kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kutoa mafunzo kwa vijana wa VETA  kuweza kuwapa mafunzo ya nishati ya jua ili waweze kuindeleza katika miji inayokua pembezoni mwa mji wa Dodoma.”

MWISHO.