RAIS
Donald Trump wa Marekani kupitia mpango wake wa kuzuia baadhi ya raia wanaotoka
nchi za kiislam kutoingia Marekani kimewakera waingereza na kusema, akizuri
Uingereza hatapatiwa mapokezi ya hadhi ya heshima ya juu ilivyo desturi.
![]() |
Rais Donald Trump wa Marekani. |
Kulingana na gazeti la
Uingereza la Daily Mail, Meya wa jiji la London Mhe Sadik Khan amesema Rais
Dolnald Trump hatapatiwa mapokezi ya hadhi ya zulia nyekundi, kama inavyofanyika kwa ma-Rais na viongozi wengine
wa hadhi ya juu wakati wa ziara yake baadae mwezi huu nchini Uingereza kwa
mwaliko wa Waziri Mkuu wa Uingereza Bi Theresa Mayor.
![]() |
Meya wa London Mhe Sadik Khan |
Meya huyo wa London amekuwa
katika vita vya maneno kwa muda mrefu na Rais huyo wa Marekani na hali imezidi
kuwa tete zaidi baada ya tukio la kigaidi lililotokea mjini Manchester Uingereza
mapema mwezi uliopita, na kisha polisi wengi kuongezwa mitaani kuimarisha
ulinzi.
Baadae Rais Trump alitoa maoni
yake kwamba hakukuwa na umuhimu wowote wa London kuweka polisi wengi kiasi kile
mitaani, jambo lililowaudhi waingereza akiwamo Meya huyo wa London.
Kulingana na taarifa
zilizoripotiwa pia hivi leo na gazeti la Daily Mail, limesema kwamba, Rais
Trump amemtumia ujumbe Waziri Mkuu wa Uingereza Bi Theresa Mayor kumtaka
acheleweshe kwa muda ziara ya mwaliko wake kwa Rais Trump nchini Uingereza
alioutoa kwake mwezi Januari mwaka huu, hadi hali ikae sawa nchini mwake.
![]() |
Watu yanao mpinga Rais Donald Trump nchini Uingereza. |
Rais Trump amemtaka Bi Theresa
Mayor pia awashauri makundi yanayo mpinga Rais Trump kuhusu ziara yake hiyo
nchini Uingereza kutoa kauli ya kuondoa pingamizi hilo ili kuwezesha ziara
hiyo, gazeti hilo limeripoti.
Mpango wa Rais Trump wa
kuzuia raia toka baadhi ya nchi za Kiislam kuingia nchini Marekani unapingwa
vikali na nchi pamoja na jumuiya za kimataifa ambapo Uingereza inaamini pia
kwamba ni mpango wa kukandamiza demokrasia duniani.
![]() |
Moja ya Raia wa Kiislam nchini Ungereza. |
Uingereza ni moja ya nchi
inayothamini haki za binadamu pamoja na kuheshimu demokrasia kwa ujumla, na pia
ni nchini yenye idadi kubwa ya raia wa kigeni walioomba uraia wa Uingereza
ambao pia wanatoka katika nchi za kiislam duniani.
(Taarifa na picha kwa
hisani ya gazeti la Daily Mail la Uingereza).
MWISHO.
No comments:
Post a Comment