LEO Jumanne Julai 18, 2017
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Saimon Sirro amefanya mabadiliko ya Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kinondoni pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga.
![]() |
IGP SIMON SIRO. |
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, kufutuatia mabadiliko hayo ya kawaida, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Suzan Salome Kaganda amekuwa Mkuu wa kitengo cha Mafao na Fidia Makao Makuu ya Polisi, na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo aliyekuwa kamanda Polisi Mkoa wa Shinyanga.
ACP MULIRO JUMANNE. |
Nafasi
ya RPC Muliro imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Sylverius
Haule, ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu wa Polisi wa Mkoa wa Mara.
Mwenyekiti
wa club ya waandishi wa Habari mkoani Shinyanga Kadama Malunde katika salamu
zake kwa Kamanda Muliro alisema,
“Club
ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (SPC), inamtakia majukumu mema RPC
Muliro ambaye amekuwa nao mkoani Shinyanga kwa kipindi chote ambacho amekuwa
akilitumikia vyema jeshi la polisi”.
SPC
imesema pia kwamba, “tunamshukuru kwa ushirikiano wote aliokuwa akitupatia kwa
muda muafaka pale tulipohitaji kulinganisha (to balance story) habari kwa
upande wa pili ili kuihabarisha na kuielimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali,
ikiwemo kutokomeza na kufichua vitendo vya kihalifu ikiwemo mauaji ya watu
wenye ualbino na vikongwe” salamu hizo zilieleza.
Akiwa
mkoani Shinyanga, Muliro alikuwa anashirikiana bega kwa bega na waandishi wa
habari na jamii kwa ujumla katika mapambano dhidi ya mimba na ndoa za utotoni, ukatili
wa kijinsia, usalama barabarani na mambo mengine kadha wa kadha na kuufanya
mkoa wa Shinyanga kuwa mahali salama pa kuishi.
SPC
iliendelea kumpongeza Kamanda Muliro na kusema, hakuwa na tabia ya kupuuzia
mambo anayoelezwa, ni mtu msikivu, siku zote amekuwa akitumia kauli ya “JIFUNZE
KUSIKILIZA”.
Salamu
hizo zilieleza pia kwamba, Kamanda Muliro mara kwa mara alikuwa akifika katika
ofisi ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (SPC) siyo tu kikazi bali hata
kubadilishana tu mawazo na kusalimiana.
SPC
katika salamu zao wamesemapia kwamba, Muliro ni kiongozi ambaye alikubali
mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia, na pia ni mtumiaji mzuri wa mitandao ya
Kijamii ikiwemo Whatsapp, na ili kuweka mawasiliano ya karibu kabisa na
waandishi wa habari, Kamanda Muliro alikubali kujiunga katika Kundi la Whatsapp
la waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga ili kurahisisha utoaji wa taarifa za
kipolisi mara tu matukio yanapotokea badala ya kujazana kwenye ofisi ya RPC.
Japo
yapo mengi ya kusema kuhusu Kamanda Muliro, itoshe tu kusema kwamba sisi
waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga hatukuona dosari kwa ndugu Muliro, tunamtakia
kila la heri katika majukumu yake katika eneo lingine hapa nchini.
Tunamkaribisha
sana Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Sylverius Haule kulitumikia jeshi
la polisi mkoa wa Shinyanga, na kumwahidi ushirikiano katikamajukumu yake,
taarifa ya SPC ilimalizia hivyo.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment