ZANZIBAR inategemewa kuwa mwenyeji wa kongamona la
kwanza la kiswahili litakalojumisha nchi wananchama wa jumuiya ya Afrika
Mashariki baadae mwezi ujao.
![]() |
Katibu
Mkuu wa Kamisheni ya Kiswahili Ukanda wa Afrika Mashariki Bw Kenneth Simala (mwenye
tai) akizungumza na waandishi wa Habari katika ukumbi wa wizara ya Habari mjini
Kikwajuni, mkoa wa Magharibi Zanzibar hivi leo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi
wa wizara ya habari wa Kikwajuni mkoani Magharibi hivi leo, Katibu Mtendaji wa
Kamisheni ya Kiswahili ukanda wa Afrika Mashariki Bw Kenneth Simala amesema Kongamano
hilo litakuwa la siku mbili.
Amesema, “Kongamano hilo linalenga kukuza
ushirikiano zaidi baina ya nchi wanachama ili kujiletea maendeleo katika ukanda
wa Afrika Mashari na linatarajiwa kuanza Septemba sita na kumalizika Septemba
saba mwaka huu.
Katibu Mkuu huyo amefafanua zaidi pia kwamba nchi
za jumuiya ya Afrika Mashariki zina haja ya kukaa pamoja na
kushirikiana kupitia lugha ya Kiswahili ili kukuza zaidi juhudi za maendeleo katika nchi husika
na kukuza uchumi wa watu wa ukanda huu, alieleza zaidi.
Aidha, amevitaka vyombo vya habari kuwa mstari
wa mbele katika matumizi mazuri ya lungha ya kiswahili na kuachana na
maneno yanayokwenda kinyume na maadili na fasihi kwa ujumla ili kisaidie kuleta
maendeleo zaidi.
Kongamano hilo linategemewa kuhudhuriwa na wadau
mbalimbali wakiwemo wanasiasa, waandishi wa habari, wasomi wa vyuo vikuu pamoja
na wajumbe kutoka nchi za Afrika ya Mashariki ambapo mada kuu ni
mabadiliko ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Kiswahili.
MWISHO.

No comments:
Post a Comment