MREMBO
Munroe Bergdorf WA Uingereza aliyejibadili jinsia toka ya kiume na kuwa ya kike
mwenye asili ya Jamaika, amewashutumu wazungu kwa ubaguzi.
![]() |
| Mrembo Munroe Bergdorf wa Uingereza. |
Bergdorf, 30, ambaye
alikuwa akiwania tuzo ya mashindano ya urembo ya L’Oreal Paris huko UK amesema
anajiona wa kipekee katika mashindano
hayo kwani ndiye wa kwanza kushiriki katika mashindano hayo baada ya
kujibadilisha jinsia.
Mrembo huyo aliyekuwa
akihojiwa na jarida la Vogue la Uingereza ameendelea kueleza kwa kulalamika
kwamba alishangaa akiwa katikati ya maandalizi ya kampeni zake za kuwania taji
hilo ndipo alipopokea email iliyomjulisha kwamba ameondolewa katika ushiriki wa
mashindano hayo.
Aliendelea kusema kuwa
baada ya kusoma taarifa hiyo alistaajabu na kuanza kulia na baadae kumfuta mama
yake na kumjulisha hayo na kuanza kulia kifuani pake huku akijilaumu kuzaliwa
mtu mweusi.
Mrembo huyo aliyekuwa
akikimbiza katika mashindano hayo alibadili jinsia yake miaka minne ambapomuda
wote kabla ya kujibadili alijulikana kwa jina la Lan. Amezaliwa na mamamwenye
asili ya Uingereza na baba mwenye asili ya Jamaika.
Mrembo huyo alimalizia kwa
kusema kwamba hakujua asili au rangi ya
mtu imeandikwa mgongoni mwake au katika damu yake au hata wakati wa kifo chake,
hivyo amewashutumu wazungu kuwa wabaguzi wa hali ya juu kwa wengine.
(Taarifa zote na picha kwa
mujibu wa gazeti la The Daily Mail la UK).
MWISHO.


No comments:
Post a Comment