MCHEZA
tenesi toka Urussi Maria Sharapova amevunja ukimya tangu alipokutwa na kashfa
ya kutumia dawa michezoni na kuwataka watu wamchukulie kama binadamu mwingine
wa kawaida.
![]() |
| Mcheza Tenesi wa Urusi Maria Sharapova akieleza hisia zake |
Sharapova, 30, alikutwa na
dhahama ya kufungiwa kushiriki mashindano yeyote ya tenesi mwezi April mwaka
huu ambapo alikuwa akitoa upinzani mkali kwenye mashindano hayo hususani
alipokuwa akikutana na mkongwe mwingine Serena
William wa Marekani.
![]() |
| Mcheza Tenesi Maria Sharapova akiwa katika ubora wake. |
Mchezaji huyo, alikuwa
akitumia dawa za kuongeza nguvu za aina ya “meldonium” kwa kipindi cha miaka
kumi mfululizo baada ya kushauriwa na daktari wake kutokana na kuwa na upungufu
wa madini ya magnesium mwilini mwake, bila kujua zitamletea matatizo michezonu,
alieleza Sharapova.
![]() |
| Maria Sharapova. |
Sharapova anasema anajiona
kuwa mfupi na mdogo mbele ya macho ya jamii japo yeye ni mrefu na kuongeza
kwamba yeye na timu yake hawakuwa na taarifa endapo madawa hayo yamepigwa
marufuku hadi vipimo vilipoonyesha.
Amewataka watu wamchukulie
kama binadamu mwingine yeyote ambaye anaweza kukutwa na masahibu katika maisha
hivyo wasimuone kama kituko, alimalizia mchezaji huyo.
(Picha na maelezo kwa hisani
ya gazeti la The Daily Mail la Uingereza).
MWISHO.



No comments:
Post a Comment