BOMU LA VITA YA PILI LATEGULIWA UJERMANI. - Mazengo360

Monday, 4 September 2017

BOMU LA VITA YA PILI LATEGULIWA UJERMANI.

Wataalamu wa kutegua mabomu mjini Frankfurt, Ujerumani siku ya Jumapili walifanikiwa kutegua bomu kubwa ambalo halikuwa limelipuka ambalo liliangushwa wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.

BOMU+VITA+YA+2
Wataalamu wa kutegua mabomu wa Ujerumani wakiwa wameketi karibu na bomu hilo Jumapili.

Bomu hilo la tani 1.4 kutoka Uingereza liligunduliwa katika eneo la ujenzi Jumatano.
Habari hizo zilipokelewa kwa shangwe na watu zaidi ya 65,000 ambao walikuwa wamehamishwa maeneo yao kwa sababu za kiusalama baada ya bomu hilo kuteguliwa.

BOMU+VITA+YA+PILI.+PX+2
Watu waliohamishwa wanatarajiwa kuruhusiwa kurejea makwao karibuni.

Hiyo ilikuwa idadi kubwa zaidi ya watu kuhamishwa tangu kutokea kwa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia nchini Ujerumani, na shughuli hiyo ilihusisha mamia ya maafisa wa serikali.
Maeneo ambayo watu walihamishwa yalikuwa katika mtaa wa Westend, na ni pamoja na hospitali kadha, nyumba za kuwatunza wagonjwa na hata katika Benki Kuu ya Ujerumani.
Inaaminika kwamba kuna mamia ya maelfu ya mabomu ya wakati wa vita ambayo hayakulipuliwa ambayo yametapakaa kote Ujerumani.
MWISHO.

(Taarifa na picha hizi ni kwa hisani ya BBC na AFP)