ASKOFU
MKUU
wa madhehebu ya Waadiventisti Wasabato Jimbo la Kusini Tanzania, Mhe Marc Walwa
Malakana ametaja Rais John Pombe Magufuli kuwa ndiye mfano wa viongozi
waadilifu na wenye hofu ya Mungu ambao bara la Afrika linawahitaji ili kuondoa
taswira mbaya iliyopo.
![]() |
RAIS Dkt John Pombe Magufuli akipokea kwa kusikiliza
kwa unyenyekevu neno la shukrani toka kwa mmoja wa waumini wa madhehebu ya
Waadiventisti Wasabato wa Kanisa la Magomeni, Jimbo la Kusini Tanzania Dkt Jim
Yonazi ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Taasisi ya Magazeti ya Serikali (TSN).
Anayeshuhudia katikati ni Askofu Mkuu wa madhehebu hayo Jimbo la Kusini
Tanzania, Mhe Marc Walwa Malakana juzi jumamosi jijini Dar es Salaam. (Picha
kwa hisani ya mpiga picha wetu).
Hayo yametamkwa mbele ya
Rais Dkt John Pombe Magufuli na Mkewe mbele ya waumini waliohudhuria katika
ibada ya sabato siku ya jumamosi iliyopita katika kanisa la Magomeni Mwembe
Chai, wilaya ya Kinondoni jijini Dar mara baada ya Rais kujumuika nao katika ibada
hiyo.
Askofu Mkuu Malakana
alisema, Rais John Magufuli ndiye Yusuf wa sasa (aliyetajwa kwenye Bibilia
Takatifu) ambaye watanzania na Bara zima la Afrika waliwahitaji sana ili kuwatoa
katika taswira mbaya ya kukosa viongozi waadilifu na wenye hofu ya Mungu.
Askofu Malakana aliendelea
kueleza kwa hisia kali kwamba, “uongozi si elimu wala akili nyingi bali ni
hekima pamoja hofu ya Mungu mtu apewayo kama zawadi toka kwa Mungu, kupitia
Roho wake, alifafanua Askofu Mkuu Malakana.
Aliendelea kusema, “Mataifa
mengi yanamwomba Mungu awapate viongozi wenye hofu ya Mungu ili watawale kwa
haki, tena wenye kumkiri yeye kwa matendo, na kumtaja moja kwa moja Rais Dkt
John Magufuli ndiye haswa wa mfano huo.
Amewataka watazania wote
kupokea zawadi hiyo toka kwa Mungu kwa kuishi maisha yenye uadilifu na hofu ya
Mungu na kusema zaidi kwamba endapo watashindwa kuishi kiuadilifu, mkono wa
sheria utawaelemea na dola itawapeleka vifungoni, alieleza zaidi Askofu
Malakana.
Nae Rais Dkt John Magufuli
amewashukuru waumini hao pamoja na viongozi wote kwa moyo wao wa uvumilivu na
upendo kwake na kusema laikusudia muda mrefu kuwatembelea na kusali nao lakini
alitingwa na shughuli zingine.
Rais Dkt Magufuli pia
alilishukuru kanisa hilo hapa nchini kwa kuisaidia vizuri serikali kutoa huduma
za kijamii kwa watu zikiwamo elimu, afya na malezi bora na kuwaomba waendelee
kufanya hivyo.
Rais Dkt Magufuli
alishindwa kujizuia furaha yake na kueleza hisia zake jinsi anavyovutiwa na
kwaya za wasabato pamoja na ujumbe unaotolewa humo na kuongeza kwamba, kinalenga
haswa dhamira ya dhati ya kumtukuza na
kumwabudu Mungu wetu, alisema Dkt Magufuli.
Rais Dkt Magufuli alienda
mbali zaidi kwa kueleza namna ya kuwatambua na kuwatofautisha waimbaji wa kwaya
za waadiventisti wasabato ikiwamo kwa kuangalia nywele zao ambazo ni tofauti
kabisa na waimbaji wa kwaya zingine.
Rais Dkt Magufuli amewaomba
wauminihaona watu wote waendelee kumwombea kwani kazi anayoifanya ni ngumu na
hivyo inahitajisana maombi ya watu na msaada wa Mungu.
Pia Rais Dkt Magufuli amechangia
ujenzi wa kanisa jipya kwa kutoa mchango wake wa mifuko mia nne ya saruji yenye
thamani ya shilingi milioni tano ambazo alizitoa na kumkabidhi Askofu Mkuu Mhe
Marc Malakana mbele ya waumini wote.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment