BOT KUZIBITI FEDHA ZA WANADAYASPORA ZANZIBAR. - Mazengo360

Wednesday, 6 September 2017

BOT KUZIBITI FEDHA ZA WANADAYASPORA ZANZIBAR.

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema inandaa utaratibu  maalum  kupitia Benki Kuu (BOT) wa kujua fedha zinazotumwa nchini  upande wa Zanzibar kutoka kwa wanadayaspora ili zichangie vya kutosha kuinua uchumi.
Image+BOT
Benki Kuu ya Tanzania (BOT).

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu kumalizika kwa kongomano la nne  la watanzania wanaoshi nje ya nchi,  Waziri wa nchi Ofisi ya Rais  na Mwemyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Mhe Issa  Haji Gavu amesema  azma ya serikali ni kuwashawishi  wanadayaspora kuja kuwekeza nchini kwa ajili ya maslahi ya nchi yao na wao wenyewe.
Ameeleza zaidi kuwa uwepo wa wanadayaspora utaleta mafanikio ya haraka  katika sekta mbalimbali ikwemo kusaidia katika nyanja za elimu na afya na kukuza zaidi ustawi wa taifa kiuchumi.
Aidha akizungumzia  kuhusu suala la utakitishaji  wa fedha haramu kwa watanzania wanaoishi nje ya nchi na wawekezaji, amesema  Zanzibar ikiwa ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga vizuri katika kukabiliana na tatizo hilo linaloisumbua dunia kwa hivi sasa, alifafanua zaidi.
Wakati huo huo Shirika la Huduma za Maktaba Zanzibar limesema linajipanga kusogeza huduma zake jirani zaidi na wilaya zote za mjini na vijijini ili kuwarahisishia wanafunzi na  wananchi wote kupata fursa ya kujisomea vitabu kwa urahisi.
Akizungumza na mwandishi wa habari Mkurugenzi wa Maktaba Zanzibar Sichana Haji Fumu amesema wananchi wengi wanoishi katika maeneo ya mbali hasa vijijini kwa kiasi kikubwa wanakosa  upatikanaji wa elimu  kwa njia ya kujisomea vitabu kutokana na umbali na uhaba wa maktaba uliopo hivi sasa.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo ameeleza kwamba ongezeko la watumiaji wa maktaba hususani kwa upande wa Pemba umeongezeka hivi sasa kutokana na uwepo wa maktaba katika wilaya  za Chake Chake, Wete na Wingwi.
Hivyo amewataka wananchi na wanafunzi kujenga utamaduni wa kuzitumia makataba zilizopo nchini ili kuongeza ufanisi na uelewa zaidi katika maisha ya kila siku.
MWISHO.