NCHI 13 za bara la Afrika na wanataaluma mbalimbali wanakutana
katika mkutano wa siku tatu mkoani Arusha kubadilisha uzoefu wa kitaaluma
kuhusu uzingatiaji wa huduma ya kisaikolojia katika malezi na makuzi bora
ya watoto na vijana.
Akifungua
mkutano huo katika ukumbi wa AICC Arusha, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee, Jinsia na Watoto Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla ameeleza
kuwa mkutano huo utatoa fursa kwa Serikali, asasi za kiraia, na wanataaluma
kutumia fursa hiyo kubadilishana uzoefu, kujenga uelewa wa pamoja kuhusu
umuhimu wa huduma ya kisaikolojia katika malezi na makuzi ya watoto na vijana
katika nchi za bara la Afrika.
Ameongeza
kuwa kuna umuhimu mkubwa kuzingatia masuala ya huduma ya kisaikojia katika maendeleo
ya mtoto kama yanavyosisitizwa katika utekelezaji wa mikataba mbalimbali ya
kimataifa ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Kimataifa wa Haki na Ustawi wa Mtoto
(CRC) na Mkataba wa Nchi za Kiafrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto (ACRWC).
“Mikataba
hiyo ya Kimataifa na Kikanda, inazitaka nchi wananchama wa umoja huo kuwa na
mifumo thabiti ya ulinzi wa mtoto dhidi ya vitendo mbalimbali vya ukatili na
unyanyasaji ili kuhakikisha utoaji wa haki na uhuru kwa mujibu wa katiba
na sheria za nchi husika” alisema Dkt Kigwangalla.
Dkt.Kigwangalla
amewakumbusha washiriki wa mkutano kuwa, ulinzi wa watoto dhidi ya vitendo vya
ukatili unakuza kwa kiwango kikubwa maendeleo ya kisaikolojia kwa mtoto
na vijana kwa kutekeleza mipango mbalimbali inayotoa kipaumbele katika kuwekeza
kwa watoto.
Aidha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi
Sihaba Nkinga amewahakikishia REPSSI kushirikiana na Wizara katika utekelezaji
wa shughuli zao ili kufikia malengo ya utoaji wa elimu na huduma ya kisaikolojia
kwa wadau wanaotoa huduma za ulinzi wa watoto.
“Tuna
waahidi ushirikiano wadau wetu katika masuala ya kumsaidia mtoto hasa mtoto wa
Kiafrika na Kitanzania katika masuala ya utoaji huduma za kisaikolojia” alisema
Bibi Sihaba
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la REPSSI Bibi Noreen Huni amewapongeza
watoto 76 kutoka nchi hizo 13 za Afrika kwa kushiriki mkutano huo wakati
REPSSI inaadhimisha miaka 15 tangu kuanzishwa kwake.
“Shirika
letu limebaini kuwa ushughulikiaji wa mahitaji ya kisaikolijia kwa watoto una
nafasi kubwa kwa Afrka kufikia malengo ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka
2030; hususani lengo namba 3, 4, 5, na 16” alisema Bibi Noren.
Mkutano
wa Kimataifa wa Malezi na mkuzi kwa wavulana,wasichana na vijana wa mwaka 2017
umeshirikisha wadau kutoka nchi 32 Duniani na unafanyika kwa siku tatu kuanzia
Septemba 04 mpaka 06 2017 ukiwa na kauli mbiu isemayo: “Haki na Usawa kwa
Wasichana na Wavulana na Vijana wote kwa ujumla”.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment